Tuesday, October 8, 2019

Halmashauri 31 zenye ofisi nje ya maeneo ya utawala Zapewa Siku 30 Kuhamia Maeneo Hayo, Vinginevyo Zitafutwa

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),  Selemani Jafo amezitaka Halmashauri 31 zenye ofisi nje ya maeneo ya utawala kuhamia katika maeneo hayo katika kipindi cha siku 30 kuanzia leo Jana Jumatatu Oktoba 7, 2019.

Taarifa iliyotolewa na mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikali Tamisemi,  Rebecca Kwandu inaeleza kuwa Jafo ametoa agizo hilo jana mkoani Rukwa baada ya kupokea maelekezo kutoka kwa Rais wa Tanzania, John Magufuli kuhusu halmashauri hizo.

Amesema halmashauri itakayozembea kutekeleza agizo hilo itafutwa.

Jafo amesema kuwa agizo hilo kutekelezwa mara moja kuanzia Oktoba 7,  2019.


from MPEKUZI https://ift.tt/2MkJVDe
via IFTTT

No comments:

Post a Comment