Friday, October 4, 2019

Lugola Awaondoa katika nyadhifa zao vigogo watatu wa Jeshi la polisi Nkasi

Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola amewaondoa katika nyadhifa zao vigogo watatu wa polisi wa Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa kwa madai ya kushindwa kutimiza majukumu yao.

Walioondolewa ni mkuu wa polisi Wilaya ya Nkasi, mkuu wa upelelezi wa Wilaya hiyo na mkuu wa kituo cha polisi Namanyere.

Taarifa iliyotolewa leo Ijumaa Oktoba 4, 2019 katika ukurasa wa mtandao wa kijamii wa Twitter ya wizara hiyo inaeleza kuwa Lugola amewasimamisha viongozi hao kwa kushindwa kudhibiti wizi wa ng'ombe 278 za wananchi na kuupuza taarifa zinaporipotiwa katika vituo cha polisi.



from MPEKUZI https://ift.tt/31L7R9b
via IFTTT

No comments:

Post a Comment