Saturday, October 12, 2019

Mwandishi Erick Kabendera ataka kuongea na DPP ili kumaliza kesi yake

Wakili Jebra Kambole  anayemtetea mwandishi wa habari nchini Tanzania, Erick Kabendera katika kesi namba 75/2019, jana ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi mwandamizi, Augustine Rwizile  kuwa wanakusudia kufanya majadiliano na ofisi ya Mwendesha mashtaka kuhusu tuhuma za uhujumu Uchumi zinazomkabili Mwandishi wa habari, Erick Kabendera.

Awali, wakili wa Serikali Wankyo Simon aliieleza  mahakama hiyo kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi bado haujakamilika. 

Alisema ni kweli jambo hilo lipo katika mchakato wa kuanza majadiliano na DPP, hivyo taratibu zikikamilika wataipa taarifa mahakama.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Octoba 24 itakapotajwa tena.


from MPEKUZI https://ift.tt/2pe3vJt
via IFTTT

No comments:

Post a Comment